Ujenzi
wa majumba ya kisasa na yenye muonekano wa kipekee unafanyika kila
siku, na biashara imetajwa kuwa sababu kubwa zaidi kwenye kuleta
ushindani.
Hapa nimekuletea list ya nyumba 5 zilizoweka rekodi ya juu zaidi kwenye bei ndani ya kipindi cha miezi 12 ya mwaka 2016.
1. Taohuayuan, Suzhou – CHINA (Zaidi ya Tsh. Bilioni 341).
Mauzo
ya jumba hili lenye ukubwa wa futi za mraba 72,441 mwezi July, 2016
yalivunja rekodi za kwenye biashara za nyumba duniani na mpaka sasa lina
rekodi ya kuwa jumba pekee lenye gharama kubwa zaidi nchini China.
Mjengo huu
una vyumba vya kulala 32, swimming pool iliyojengwa kama ziwa lenye
maji mengi, sehemu ya kukinga Wine, pamoja na bustani za kila aina,
jumba hili liliwahi kutajwa na shirika la Umoja wa Mataifa la
Elimu UNESCO kama bustani bora ya dunia
2. 301 N Carolwood Drive, California – MAREKANI (Zaidi ya Tsh. Bilioni 222).
Mjengo
mwingine nii huu kutoka California, uko kwenye eneo la ukubwa wa futi
za mraba 30,000 huko Los Angeles, uliuzwa kwa bilionea Tom Gores
mwezi October 2016. Una vyumba 10 vya kulala, bafu 20, uwanja wa
Basketball, gereji 10 na hapo ulikuwa umepungzwa kwa dola milioni 50
kutoka bei ya mwanzo.
3. The Playboy Mansion, California – MAREKANI (Zaidi ya Tsh. Bilioni 222).
Wakati watu wakishangaa bei iliyotangazwa juu ya kuuzwa nyumba hii ambayo ilikuwa zaidi ya dola za Marekani Milioni 200m,
alijitokeza bilionea Daren Metropoulos na kuinunua kwa dola milioni 100
mwezi August 2016. Ndani yake kuna ukumbi wa kisasa wa Cinema, nyumba
ya pembeni kwaajili ya wageni, Zoo yenye leseni kwaajili kuhifadhi
wanyama pori.
4. Crespi Hicks Estate, Texas – MAREKANI (Zaidi ya Tsh. Bilioni 222).
Likiwa
limepambwa na sakafu ya Mable kwenye njia zake, hili lilikuwa jumba
lililouzwa bei kubwa zaidi kwenye mji wa California, Marekani. Jengo
hili liko kwenye eneo la ukubwa wa futi za mraba 28,000 huko Dallas na
lilinunuliwa na muanzilishi wa kampuni ya Beal Bank, Andrew Beal
mwezi January 2016.
Pamoja na muonekano wa ukubwa huo lina vyumba 7 tu vya kulala. Pia inatenganisha nyumba ya wageni na wenyeji.
5. The Penthouse, 432 Park Avenue, New York – MAREKANI (Zaidi ya Tsh. Bilioni 194).
Hii
ni nyumba ya ndani (Apartment) iliyoweka rekodi ya mauzo makubwa
jijini New York Marekani mwaka 2016. Ikiwa ndani ya eneo la ukubwa wa
futi 8,255 za mraba ndani ya jengo refu zaidi la makazi ya watu jijini
humo, Michoro ya ramani zake imebuniwa na mtaalamu wa majengo Rafael
Viñoly, ilinunuliwa na bilionea kutoka Saudi Arabia, Fawaz Al Hokair.
No comments:
Post a Comment